MBUNGE WA MONDULI AFUNGUTKA SAKATA LA HIFADHI YA NGORONGORO


Mbunge wa Monduli amesema Wamasai wa Ngorongoro ni Watanzania na wana HAKI sawa kama Watanzania wengine. Tofauti kubwa ni kabila letu  kulinda utamaduni wetu ambao pia umekuwa kivutio kikubwa cha utalii ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro. 

Naamini Watanzania wote tunafahamu heshima hii ya Ngorongoro Crater kama moja ya maajabu ya dunia na mtaji mkubwa sana kiuchumi kwa Nchi yetu.

Nadhani ni muda sahihi   kwa Serikali  kuiwezesha Mamlaka ya Hifadhi ya NgoroNgoro ili kulinda hifadhi yetu na kurejesha mahusiano mazuri ya wanyama na binadamu kama ambavyo imekuwa tangu kuanzishwa kwa hifadhi hii mwaka 1959.

Hoja ya wingi wa mifugo na zozote zingine zinajadilika kukiwa na mahusiano mazuri na wananchi na tunaiamini Serikali Mama Samia Saluhu Hassan ni sikivu.

Previous Post Next Post