TWCC KUWEZESHA WANAWAKE NA VIJANA KUSHIRIKI KWENYE FURSA ZA MANUNUZI

 



Na Humphrey Msechu, DAR ES SALAAM

CHEMBA  ya wafanyabiashara wanawake Tanzania TWCC imesema itahakikisha  inawaweezesha wanachama wake  wanawake na vijana kuweza kuongeza ushiriki katika fursa za manunuzi ndani ya serikali na sekta binafsi zitakazowasaidia kujikwamua katika biashara.



Kauli hiyo imetolewa leo  jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi Mtendaji wa TWCC Mwajuma Hamza wakati wa warsha ya siku moja ya  vijana na wanawake  wafanyabiashara  na kufafanua kuwa Twcc ina   matarajio makubwa kutoka kwa wanawake na vijana  katika kuhakikisha wanakuza na kuinua biashara  nchini.



Mwajuma amefafanua kuwa  Serikali imejipambanua na imejiweka wazi kwenye progamu ya manunuzi ya umma na kupata fursa zilizopo kwa kuwajengea uwezo vijana na wanawake.



Nao baadhi ya washiriki wa kongamano hilo wamesema  kuwa kila mtu anapofanya vizuri katika biashara ni kutokana na ufanyaji wake wa kazi unapelekea kupata tenda za kutosha kutoka katika sekta za umma na binafsi  na mwenyekiti wa Bunju Women Jacqueline Mkina ameishukuru TWCC kwa mafunzo wanayowapatia kuhusiana na tenda na pia kuwawezesha kufahamu wapi pa kuchukua mtaji kwenye mabenki itakayokusaidia kufanyakazi.





Previous Post Next Post