Na Lilian Ekonga, Dar es salaam.
Meneje Programu wa Asasi za Kiraia (FCS) Nasim Losai ameiomba serikali iangazie katika kuwawezesha makundi maalumu katika kuweza kufikia miundombinu ya kidigitali ili waweze kufanya maamuzi sahii na kushiriki katika michakato ya maendeleo na kuimarisha uchumi wao.
Hayo ameyasema leo Agust 12 katika Mkutano wa kitaifa wa watu wenye ulemavu, madiwani na wadau uliofanyika jiji la Dar es salaam.
Ambapo amesema mkutano huo umejikita katika kuangazia ushiriki wa watu wenye ulemavu katika maendeleo, uchumi na kijamii huku ukiangazia matumizi ya takwimu za sensa katika kuboresha mapango wa halmashauri za wilaya na ngazi za kata.
"Serikali imekuwa sikivu na sana na sisi foundation tunazaidi ya miak 20 tumekuwa tukisaidia serikali hasa katika shughuli za kutetea watu wenye ulemavu na michakato ya kiserikali hasa kwenye majengo mengi sana mioundombinu imebadilika na kazi kubwa imefanywa na fsc pamoja na makundi haya" amsema Losai
Kwa upande wake Peter charlse Mshauri wa kiutalamu wa maswala ya watu wenye ulemavu Tanzania amesema mkutano huo umejuisha watu mwenye ulemavu 600 kutoka ndani ya jiji la Dar es salaam wakiwepo madiwani 60 wa viti maalimu na wakuteuliwa.
Ameongeza kuwa Malengo ya mkutano huo ni kuwajengea uelewa watu wenye ulemavu katika maswala ya sensa, uchumi na fursa na utakwenda kuangazia zaidi maswala ya uchumi na kuona fursa zipi walemavu wameweza kushirikishwa na wao wameweza
"Ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu bado ni mdogo ndomana wakamamuu kuwalika madiwani katika mkutano huo ili kuangalia changamoto ipi wapi na kuwajengea uwezo madiwani ili kuweza kuwashirikisha madiwani katika mipango yao ya maendeleo kupitia mabaraza yao ndani ya halmashauri" amesema
Nae Hamadi Abdallah komboza, mwenyekiti wa Taifa wa chama cha walemavu Tanzani amesema changamoto kubwa kwa watu wenye ulemavu ni maswala mazima ya ajira huku akimuomba kamshina wa kazi na vyama venye ulemavu kufanya ukaguzi kwenye mashirika na taasisi ambazi zinapasqa kuajiri watu wenye ulemavu lakini bado hazija kidhi ili kuweza lueta msukumo zipelekwa mahakamani ikibidi ili watu wenye ulemavu waweza kuajiriwa.
Jonas Lubalo, katibu mkuu shirikisho la vyama vyenye ulemavu Tanzania amesema Wanaishuru Taasis ya Ikupa Trust Fund kwa kuendelea kuchangia kutoa huduma za kwa watu wenye ulemavu kwa namna anavyotoa misaada kwenye maeneo mbalimbali ya watu wenye ulemavu.