DKT. BITEKO ASHIRIKI KONGAMANO LA NISHATI SAFI YA KUPIKIA ZANZIBAR


Na mwandishi wetu
 
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe Dkt. Doto leo Agosti 23, 2024 anashiriki Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia linalofanyika katika Hoteli ya Kwanza, Kizimkazi-Zanzibar.

Kabla ya kushiriki Kongamano hilo, Dkt.Biteko alitembelea Mabanda ya Maonesho ya Wadau wa Sekta ya Nishati Safi ya Kupikia ambao wanatoa elimu ya matumizi ya nishati hiyo na  teknolojia zake.

Kaulimbiu "Upishi Salama kwa Afya ya Mpishi na kwa Maendeleo ya Jamii"
Previous Post Next Post