SERIKALI KUBORESHA MAZINGIRA YA VIWANDA NA MIUNDOMBINU YA UCHUKUZI KATIKA KUKUZA BIASHARA NCHINI


Na Lilian Ekonga, jijini Dar es salaam

Serikali  itaendelea kuboresha mazingira ya viwanda ikiwa na pamoja kuimarisha upatikaji wa nishati ya umeme wa uhakika na kwa bei nafuu, kujenga  barabara , reli na viwanja vya ndege, bandari  na miundombinu mengine ya uchuzi ili kuweza kukuza wizara ya biashara.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Biashara  na Maendeleo ya viwanda Zanzibar, Mhe Omar Said  Shaaban wakati akifungua Maonesho  ya Saba  ya Bidhaa za viwanda  vya Tanzania yanofanyika katika viwanja vya sabasaba  jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 3 Disemba hadi 9 yanoratibiwa  na Mamlaka ya maendeleo ya biashara Tanzania(Tantrade).

Waziri amesema kuwa  serikali itaendelea kusimamia tantrade  katika kutekeleza majukumu yake ili waweze kuongeza kasi  zaidi ya kuendeleza na kukuza biashara nchini.


"Naagiza tantrade kushirikiana na idara za biashara nchini zilizipo katika ofisi zetu za tawala za mikoa katika kuwafikia wenye viwanda kwa lengo la kuwaunganisha na masoko kutoa programu za uendeshaji na ukuzaji biashara na fursa mbalimbali zilizopo nchini" amesema waziri Omar.

Aidha ametoa wito kwa wasomi na watafiti kufanya tafiti zitakazo  saidia viwanda nyetu kuimarika kwa kutumia mazingira halisi ya Kitanzania.

Pia waziri ametoa wito kwa washiriki wa maonyesho hayo kuyatumia  ipasavyo ili kuweza  kutangaza technolojia ya viwanda vidogo, vya kati na viwanda vikubwa.

"Nimefarajirika sana tantrade imefanya jitihada za kuwaanganisha wazalishaji na technolojia  ufunganisha wa bidhaa na kuratibu misafara ya kibiashara  katika wa nchi mbalimbali" amesema Waziri

Kwa upande wake  Mkurugenzi Mkuu wa Tantrade, Bi Latifa Khamisi amesema maonyesho hayo yanakutanisha wadau 502 katika sekta za uzalishaji , kilimo, uvuvi, mifugi na bidhaa za viwandani za technolojia mbalimbali.
Previous Post Next Post