PROF MKENDA: WANAOJIHUSISHA NA VITENDO VYA UDANGANYIFU WA MITIHANI WAFUNGWE JELA


Na lilian Ekonga. Jijini Dar es salaam.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, ametoa onyo kwa wasimamizi wote wa mitihani  na watumishi wa serikali  kuanzia ngazi za  maafisa Elimu wa mikoa, wilaya na walimu wanaojihusisha na vitendo vya  udanganyifu wa  mtihani wafungwe  na wakae ndani hata kwan miez sita tuu lakini wasipigwe faini ili ije kuwa fundisho kwa wengine.

Waziri ametoa kauli Hiyo leo Disemba 5 jijini Dar es salaam, ambapo amesema watapitia sheria zao na kuhakikisha kwamba kama kuna upenyo unaowezesha watu wafanye udanganyifu kwenye mitihani na wakatoka  bila kuchukuliwa hatua yoyote watapeleka mapendekezo ya kufanya mabadiliko ili yoyote anayechezea mtihani wala asipigwe faini afungwe jela.

Waziri Mkenda amesema kuwa Wataongea na mamlaka husika kwamba wasiwe wanawafukuza tuuh kazi bali wanachofanya ni kitendo cha  jinai na ukiangalia garama za kuendesha mitihani ni kubwa sana na  mtu anayevuruga mitihani  anahujumu uchumi wa nchi yetu.

"Nisisitize kwamba kuna kauli inasema ukitaka kuua taifa ua Elimu haribu elimu ya nchi ile, Na sasa hivi tunafanya mageuzi ya elimu hapa nchini sera mitaala haiondoi jukumu la kusimamia kwamba elimu tunayoitoa sasa hivi tunaitoa kwa tararibu zinazo kubalika sio kwa mtu kwenda kufanya udanganyifu katika mitihani."amesema prof Mkenda.

Ameongeza kuwa wataendelea kuongea na mamlaka kwamba watu hawa wachukuliwe hatua kwa kuwafukuza kazi au kuwasimamisha kazi washitakiwe mahakamani wahukumiwe na waende jela. 

 "Waache kufundisha watoto  rushwa, udanganyifu na taifa letu halita endelea kwa kuwafundisha watoto wetu udanganyifu na swala la mitihani hawata kuwa namchezo nalo wataendele kukaza buti na wanaopanga kufanya hivyo wajue kwamba watawakanata  tuu."amesema Waziri

"Tutaendelea kuongea na mamlaka kwamba watu hawa wachukuliwe hatua kwa kuwafukuza kazi au kuwasimamisha kazi washitakiwe mahakamani wahukumiwe na waende jela,"amesema. 

Amesema  udanganyifu huo unatokea pale kwenye kituo cha kufanyia mitihani mara nyingi na wameweza kunasa shule mbali mbali ambopo wasimamizi pamoja na walimu wa pale wameshirikiana kwa namna moja ama nyingine kufanya udanganyifu katika mitihani.
Previous Post Next Post