WAZIRI WA FEDHA MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI 15 YA CHUO CHA KODI


Na Lilian Ekonga Dar es salaaam. 

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Mwigulu Nchemba  anatarijiwa kuwa mgeni  Rasmi katika Mahafali 15 ya chuo cha kodi (ITA) ambapo atatunuku vyeti vya stashahada, Shahada na stashahada ya Uzamili kwa wahitimu 489 kutoka chuo hapo 

Hayo yamesemwa Leo  November 23  na Mkuu wa Chuo Cha Kodi, Prof Isaya Jairo wakati akizungumza na waandishi wa Habari ambapo amesema Mahafali hayo yatanyika tarehe 25 novemba 2022 jijini Dar es salaam katika ukumbi uliopo chuoni hapo kuanzia saa tatu Hasubuhi. 

 "Kuna ongezeko la asimilia  25.1 ya ya wahitimu kwa mwaka huu 2022 ukilinganisha na wahitimu 387 ambapo walihitimu mwaka 2021, ongezeko hili linatokana na jitihada za chuo  kuhakikisha viwango vya mafunzo yanayotolewa na chuo vinakidhi matakwa ya mahitaji ya taaluma na kodi" amesema Prof Isaya.


Ameongeza kwa kuzingatia mahusiano na ushirikiano uliopo kati ya Chuo na Mamlaka za Mapato za Afrika chuo kimewaalika baadhi ya wakuu wa Mamlaka za Mapato mbalimbali ambapo tayari baadhi wamethibitisha Kushiriki.

Aidha amesema Chuo cha kodi kinatoa mafunzo yanayoendana na mabadiliko ya sayansi, teknolojia na uchumi yanayolenga mahitaji ya soko la wataalamu katika nyanja za forodha na kodi hapa nchini na barani Afrika.

"Nachukua Fursa Hii kuwakaribisha, wageni waalikwa wote , wahitimu  pamoja na wazazi katika Mahafali haya ya 15 ya chuo cha Kodi," Amesema.
Previous Post Next Post