AIRTEL WAJA NA OFFER NZITO MSIMU WA SIKUKUU KWA WATEJA WAKE



Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kupitia huduma yake ya Airtel Money leo

imeutangazia umma kuwa wateja wa Airtel Money wataendelea kutuma pesa bila makato - FREE

msimu huu wa sikukuu.


Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchunda alisema,

"Kupitia huduma yetu ya Airtel Money tunaendelea kuwapa wateja wetu wote uhakika kuwa

wataendelea kufaidika na huduma ya tuma pesa popote nchini Airtel kwenda Airtel. Tuma pesa

BURE inaendelea kuwadhihirishia wateja kuwa dhamira yetu ya kuwafikishia wateja wetu

huduma zakifedha kidigitali iko palepale, huduma hii imekuja wakati muafaka kwa kuwa watu

wengi wanatuma pesa nyumbani kwaajili ya maandalizi ya shamrashamra za kusheherekea

sikukuu za chrismasi na Mwisho wa mwaka.



"Tunayo furaha kutangaza Habari Njema hii kwa wakati huu ambao huduma hii inahitajika kila

siku hasa kwa maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma za kibenki. Airtel Money inapatikana kila

kona

"Mteja anaweza kutuma kiasi chochote BURE atakachokatwa ni tozo ya serikali tu kwa mujibu

wa utaratibu wa huduma za kifedha kwa njia ya mtandao lakini sisi Airtel Money hatutakuwa na

nyongeza au makato yoyote kwa mteja wetu" aliongeza Nchunda

"Airtel pia katika msimu huu tunaendelea na kupanua mtandao wetu zaidi kwa kufungua maduka

mengi zaidi ya Airtel Money Braches pamoja na huduma ya 4G nchini kote. Tunaendelea kupanua

wingo wa huduma ya 4G kwa kuongeza minara zaidi na hii itafanya mtandao wa Airtel kuendelea

kupatikana kwa urahisi na hivyo kuwafanya wateja wetu kuendelea kufurahia huduma iliyo bora

zaidi, alisema Nchunda huku akiongeza kuwa ili mteja kufurahi huduma hii kutuma pesa bure

Airtel kwenda Airtel atapiga *150*60# changua Tuma Pesa bure.

Airtel Money imekuwa ikizindua huduma na bidhaa ambazo ni zakibunifu zinazopatikana kwa

urahisi kwa kutoa huduma ya mikopo binafsi ya - Timiza Loans, mikopo ya vikundi - Timiza Vicoba

loans huku ikiwa imeunganishwa na huduma za benki zaidi ya 40 hapa nchini na hivyo kuweza

kufanya miamala kutoka kwenye akaunti ya benki kwenda kwenye Airtel Money papo kwa hapo'.

Previous Post Next Post