LSF YAZINDUA MTANDAO WA KIDIGITALI WA MSAADA WA KISHERIA 'HAKI YANGU'





Na Lilian Ekonga.....

Katika kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata huduma ya msaada wa kisheria bila kujali wapi alipo, Asasi isiyo ya Kiserikali ya Legal Services Facility (LSF) kwa kushirikiana na kampuni ya kiteknolojia ya TechForward wamezindua rasmi mtandao wa kidigitali wa msaada wa kisheria unaoitwa 'HAKI YANGU' chat bot.


Akizungumza katika hafla  uzinduzi  Mkurugenzi Mtendaji wa LSF, Bi. Lulu Ng’wanakilala, amesema Mfumo huo  unaendeshwa kwa akili Bandia AI ikibuniwa mahususi kusaidia wasaidizi wa kisheria na wananchi kupata huduma za msaada wa kisheria kwa wakati,usahihi na usalama.

"Kupitia jukwaa hili wasaidizi wa kisheria watakuwa  na ufikiaji wa taarifa sahihi za kisheria kwa masaa 24 siku yoyote  popote pale walipo, wananchi wataweza kuwasiliana na mfumo  wenye akili bandia unaoelewa maswali yao ya kisheria na kuwaunganisha na njia za rufaa  pale ambapo kesi inazidi uwezo  wa  mtoa huduma za msaada wa kisheria.



Ameongeza  kuwa Mfumo huo umejengewa maudhui ya kisheria yaliyohakikiwa  na njia za msaada na  kuhakikisha  hakuna anayebaki nyuma  hususani wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na jamii  ambazo hazipati huduma zinazohitaji.


Kwa upande wa Serikali, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA (ICT Commission), Dkt. Nkundwe Mwasaga, alieleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya usambazaji wa mtandao katika maeneo ya vijijini ili kuhakikisha huduma kama hizi zinamfikia kila Mtanzania.



" Serikali inajenga minara zaid ya 750 ili huduma ziwafikie watu wengi ambapo itasidia huduma iweze kuwafikia watu wengi zaidi ambapo idadi ya simu janja inakuwa zaidi kutoka na takwimu ya TCRA inasema simu janja zipo milioni 24" amesema  Mwasanga.


Awali akizungumza  Mkurugenzi Mtendaji wa TechForward, Bw. Elias Patric, amesema  'HAKI YANGU' chat bot  inakipengele kinachomuwezeaha   mtumiaji kuunganishwa na mtoa huduma za msaada wa kisheria  aliyekaribu kili kupata msaada wa kisheria bila malipo karibu na anapoishi.

"Programu hiyo inapatikana kupitia simu janja au kompyuta, na inatoa huduma kwa lugha rahisi na rafiki kwa mtumiaji ya kiswahili Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa kila mmoja, hususan wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, wanaweza kufikia haki bila vikwazo" amesema






Previous Post Next Post