Na Lilian Ekonga
Katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 serikali imeshauriwa kutenga Bajeti kwa ajili ya kutoa mafunzo kazini kwa walimu waliopo ili waweze kusaidia utekelezaji wa tahasusi na kuajiri walimu wapya wenye ujuzi umahairi katika tahasusi husika.
Hayo ameyasema , Mkurugenz Mtendaji wa Hakieleimu Dkt John Kalage, wakati akitoa mapendekezo juu ya upangaji na utendaji bajeti ya sekta ya Elimu ya Mwaka wa Fedha 2024/25 leo aprili 23, 2024 jijin Dar es salaam.
"Ikumbukwe kuwa Hadi Februari, 2023 mahitaji ya walimu katika shule za sekondari yalikuwa ni 174,632 ambapo walimu waliopo ni 84,700 na upungufu wa walimu 89,932 sawa na asilimka 51.5%" amesema Dkt Kalege.
Pia Haki Elimu wameshauri uwepo mpango maalumu wa kuhamasisha udahili wa wanafunzi wa ualimi vyuoni ili kuendelea kutengenezq walimu wenye ujuzi mahususi kulinganq na mabadiliko ya tahasusi.
Aidha wameiomba serikali kutenga bajeti maalum kwajili ya uchapaji nq usambazaji wa vitabu vya kiada mashuleni kwa kuzingatia vitabu hivyo ni vipya na havina akiba ya vitabu mbadala.
"Kuweka Mpango maalumu wa usambazaji wa vitabu hivi mashuleni ukianisha muda mahususi wa ukamilishaji wa zoezi hili" amesema.
Mbali na hayo, Hakielimu wamependekeza ujumuishi wa teknolojia katika utekelezaji wa mtaala mpya wa Elimu, ambapo imeishauri serikali kupitia Wizara za Sekta ya elimu kutenga Bajeti kwaajili ya uboreshaji wa miundombinu ya shule ya msingi na sekondari ili kuziandaa na utoaji wa Elimu kwa Mtaala mpya na matumizi ya teknolojia.
Vilevile HakiElimu imependekeza Serikali itenge Bajeti kwaajili ya ununuzi wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia vya teknolojia lakini pia kuanzisha vipindi vya ujuzi wa matumizi ya mtandao ili kuwawezesha wanafunzi kuwa na umahiri wa kutumia mtandao kwa usahihi, uwezo wa kutatua matatizo na uwezo wa kujifunzia.