MBIO ZA 'PANDE TRAIL RUNNING & CYCLING' ZA KUSAIDIA WATOTO WENYE ULEMAVU KUFANYIKA KESHO NOV 19


Na Andrew Chale,
Dar es salaam.

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Mary Masanja anatarajiwa kushiriki tamasha la mbio za hisani za 'Pande Trail Running & Cycling'
Novemba 19 mwaka huu zenye lengo la kuwasaidia watoto wenye ulemavu wanaoishi mitaa inayozunguka Pori la akiba la Pande lililochini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wananyapori nchini (TAWA).

Mh. Mary Masanja atashiriki mbio hizo pamoja na wadau mbali mbali ambapo pia atakabidhi badhi ya vifaa kwa watoto hao.

Kwa mujibu wa Afisa Mahusiano Mkuu wa TAWA, Vicky Kamata, amesema kuwa shughuli hiyo ya kipekee katika Pori la Pande
zimeandaliwa kwa pamoja na TAWA kwa kushirikiana wadau ambao ni Dar Running Club na Taasisi ya Africa Foundation for inclusive Communities (AFIC) ikiwa na lengo kusaidia watoto hao hususani walemavu.

Ambapo kutakuwa na Michezo mbalimbali ikiwemo ya kuendesha Baiskeri na kukimbia katika maeneo hayo yenye Utalii wa msitu huo wa Pande.


"Maandalizi yanaendelea vizuri na Naibu Waziri Mhe. Mary Masanja ndiye atakae kabidhi vifaa hivyo katika hilo la tarehe 19.11.2022." Alisema Vicky Kamata 

Na kuongeza kuwa:
"Mbio hizi tumezipa kauli mbiu ya "Kimbia Mlemavu atembee", hivyo tuungane na Naibu waziri Mhe Mary Masanja, tuungane na TAWA,tuungane na Watoto wenye Ulemavu katika kushiriki Mbio hizi." Alisema.

 Aidha, alisema zoezi la usajili lilikuwa likiendelea Mlimani City, ambapo pia unaweza piga simu: 0788466330 na
0713974398 kwa maelezo zaidi.

Ambapo vifaa vya mazeozi vitanunuliwa kwa ajili ya watoto 36 wenye ulemavu wa miguu ambapo Watoto hao wenye ulemavu wanasimamiwa na Taasisi ya Africa Foundation for Inclusive Communities (AFIC).

Pia mbali na mbio hizo, kutakuwa na mambo mengine mengi kwa washiriki ikiwemo michezo na nyama choma za pori 

Previous Post Next Post