Na mwandishi wetu
ZAIDI ya Mabalozi 62 na wanadiplomasia wanatarajia kushiriki mbio za Marathon za kilometa 5 hadi km15 zinazo tarajia kuanza Mei18 Mwaka huu katika Daraja Tanzanate,Mtaa wa Baraka Obama hadi Masaki jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Waandishi Habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ally Bujiku amesema kuwa Mbio hizo za Afrika Marathon zinalenga kuadhimisha miaka 61ya Maadhisho ya Nchi huru za Umoja wa Afrika ambapo lengo mbio hizo ni kukuza Diplomasia katika sekta ya Michezo.
"Michezo ni Biashara,ni Ajira ni kazi pia ni Diplomasia,Tumechagua Riadha kwasababu kila mtu Anaweza kushiriki"Alisema Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Wizara ya Mambo ya nje Balozi Ally Bujiku.
Balozi Bujiku aliongeza kuwa Sambamba na Mbio hizo pia kutakuwa na Chakula chapamoja katika Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam.
Aidha,Balozi wa Somalia Nchini Tanzania YassiniAlly khali amesema yupo tayari kukimbia kilometa 15 zitakazo anza ukumbi wa Mwalimu Nyerere hadi Masaki.
kwa upande wa Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mindi kasiga amesema mbio hizo zinatarajiwa kuhudhuriwa wanariadha na kama vile Filbart Bayi Juma ikanga Magedalena.
"Pia shule mbalimbali zinatarajiwa kushiriki ikiwemo Pugu,Uhuru Mchanganyiko,Pamoja Jangwani sekondari"Amesema Mkuu wa kitengo cha Mawasilano wizara ya mambo ya nje Mindi kasiga.