SHIRIKA LA FCS WAMESAINI MKATABA NA TAASISI YA TRADE MARK AFRIKA, WANAWAKE, WALEMAVU KUNUFAIKA


Na Lilian Ekonga, Dar es salaam.

Shirika la Foundation Civil of sociefy (FCS) wamesaini makataba wa mradi na Taasisi ya Trade Mark Afrika kwa miaka mitatu wenye thamani ya bilioni 2.3 kwa  lengo la kuongeza   ushiriki wa azaki katika kuboresha ulinzi  mlaji na kusaidia biashara iwe jumuisha na endelevu.


AKizungumza na waandishi wa habari mei 14, Mkurugenzi wa FCS, Justice Rutenge amesema mradi utasadia sana katika ulinzi wa walaji kwa upande wa haki pamoja na wajibu wa mlaji na  wapi kwa  kupeleka mapendekezi kwa bidhaa anayoitumia.

"Sisi kama fsc tutaimarishi ushiriki wa asasi za kiraia kwenye maswala ambayo yanahusu ulinzi wa walaji, azaki zitasaidia kuibua, maoni mapendekezo, malalamiko ikhitajika hatua ya kupeleka madai kwa vyombo mbalimbal8 ili yaweze kufanyiwa ufumbuzi na mlaji aweze kulidwa"amesema Rutenge.

Pia amesema  mradi huo utasaidia kuongeza ujumuishi na muendelezo kwenye biashara kwq kuongeza fursa za biashara kwa wanawake,vijana na walemavu.


"Mradi utawawezeha wanawake kuchangamkia fursa hasa katika  matumizi ya gesi safi  ya kupikia ,kuuza majiko ili waweze kujipatia kipato na  kusaidia nchi katika kuendana  amabadiliko ya tabia ya nchi" amesema

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Trade Mark Africa, Elibariki shammy amesema  wameungana na  asasi za kwa kirai kwa lengo la   serikali iweze  kujua mambo gani yabadilishwe ili  wananchi waweza kupata bidhaa kwa bei inayo stahili na waweze kujengea uwezo  kutoa elimu kwa wajali na kupata bidhaa zilizo salama zaidi


Aidha amesema mradi huo utaweza kuwawesha wanawake,vijana , wenyeulemavu  kuona wanawezaje kuwezesha zaidi kuingia kwenye biashara.

"Kujengea uwezo asasi ya kirai kunaweza kuasidia bidhaa za kitanzania kuweza kushindana katika masoko ya nje" amesema
Previous Post Next Post