Zaidi ya washiriki sitini wanatarajia kushiriki mashindano ya mbio za pikipiki yaliyopewa jina la East Afrika Sun Village Enduro Racing 3.
Akizungumza kuelekea siku ya Mchezo huo Mratibu wa Mashindano hayo ambaye ni Mwenyekiti wa Dar es Salaam Riders Motor Sports Club ( DRMSC) Ahmed Abdallah amesema mchezo huo unalengo la kuwaleta karibu wadau wa michezo ya Mbio za Pikipiki na kuionyesha Dunia kuwa Tanzania kuwa ni miongoni mwa Washindani katika mchezo huo.
Aidha Ahmedi Abdallah ameongeza kuwa mashindano hayo ya Mbio za Pikipiki ya Sun Village Enduro 3 yatafanyika Kibaha Misugugugu yakishirikisha pikipiki maalum za Mashindano pamoja na Bodada huku washirki wakitarajiwa kupita na vyombo vyao moto katika barabara za Mchanga, Tope, pamoja na Matuta Makubwa .
Sanjari na hayo Mwenyekiti DRMSC Ahmed Abdallah amesema mashindano ya mchezo huo yanatarajiwa kufanyika Julai 17,2022 katika viwanja vya Misugusugu Shule Kibaha huku yakishirikisha washiriki kutoka Mikoa mbalimbali ikiwemo mkoa wa Morogoro , Dar es Salaam , Arusha , Pwani na Zanzibar .